UPUNGUFU
HomeHope for Today (Swahili) › Episode

UPUNGUFU

10:30 Jul 14, 2023
About this episode
MATUMAINI PROG 1508 TITLE: UPUNGUFU TEXT: WAGALATIA 4:8-14 Hujambo na karibu tujifunze neno la mungu pamoja leo twalichambua fungu la neno kutoka wagaltia 4:8-14 UPUNGUFU Jina langu ni David Mungai, wimbo alafu tuendelee WIMBO Naam karibu ten tujifunze neno la mungu, upungufu mmoja wapo wa mambo yaliyo na upungufuni dini na zaidishirika za waumini zilizo na ufisadi. Tumefisadihata nainjili tunapoiuza injili twaifisadi maana wokovu ni kwa Imani katika yesu kristo tunapoongeza madoido yetu katika injili ya bwana wetu yesu kristo twafisadi na tunakuwa na upungufu nasoma sasa neno kutoka waraka wa Paulo kwa wagalatia 4:8-14 8 Lakini wakati ule, kwa kuwa hamkumjua Mungu, mliwatumikia wao ambao kwa asili si miungu. 9 Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? 10 Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka. 11 Nawachelea, isiwe labda nimejitaabisha bure kwa ajili yenu. 12 Ndugu zangu, nawasihi, iweni kama mimi, maana mimi ni kama ninyi. Hamkunidhulumu kwa lo lote. 13 Lakini mwajua ya kuwa naliwahubiri Injili mara ya kwanza kwa sababu ya udhaifu wa mwili; 14 na jaribu lililowapata katika mwili wangu hamkulidharau wala kulikataa, bali mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama Kristo Yesu. Paulo alikasirishwa na wakristo wa Galatia kwa wakristo wa Galatia kwa sababu hapo mbeleni waliabudu miungu yao wenyewe walichonga wenyewe kwa mikono yao halafu wakaabudu Kilichomkasirisha Paulo sana ni kwamba baada ya kumwamini Yesu Kristo baadhi yao walitamani kurudia kuabudu miungusanamu walichinga kwa mikono yao hata mungu alikasirishwa nasi tunapotamani kuyarusia ya zamani mahirizi ya zamani mahirizi upigaji wa ramli uchawi na kadhalika Yesu alisema ni kama ngurue anayerudia matapiko yake ni chukizo kwake mungu pamoja na hayo, Pauloaliwakemea wagalatia kwa kuzingatia sana siku kwa sababu za kidini wazitukuza siku kuliko mungu muuba wa sile siku. Hakuna chochote siku, miaka, kilicho hai milima n ahata mabonde yaliyopita yaliyopo na yajayo hakuna kinachopaswa kuabudiwa ila yesu kristo mungu baba na mungu roho mtakatifu ni amri na twapaswa kuitii. Siku si kubwa kuliko aliyeiumba ilesiku Jambo la tatu ingawa Paulo aliwakemea sana wagalatia aliwakemea akiwarudi kwa sababu ya upendo wa kristo 12 Ndugu zangu, nawasihi, iweni kama mimi, maana mimi ni kama ninyi. Hamkunidhulumu kwa lo lote. 13 Lakini mwajua ya kuwa naliwahubiri Injili mara ya kwanza kwa sababu ya udhaifu wa mwili; 14 na jaribu lililowapata katika mwili wangu hamkulidharau wala kulikataa, bali mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama Kristo Yesu. Heri ndugu au dada anayewarudisha wengine katika ushirika kwa upendo na tumuige ndugu yetu Paulo Twarejesha ndugu na dada walioangukia dhambini kwa upendo upendo wa kristo unaotupenda nana tulivyo OMBI Ingawa wahitaji msaada wetu, tafadhali wasiliana nasi, anwani na nambari ya simu ntaisoma baada ya wimbo huu
Select an episode
0:00 0:00